(DCEA)
Nyumba za upataji nafuu ni nini?
Ni Sehemu ambayo huwasaidia waraibu ambao bado wako kwenye matumizi ya vilevi kuachana navyo au kupata nafuu kwa kutumia hatua 12 za upataji nafuu pamoja na unasihi.
Huduma katika nyumba za upataji nafuu huendeshwa na asasi za kiraia ambapo waraibu wa dawa za kulevya wanapata huduma kwakupitishwa kwenye hatua hizo bila kutumia dawa ya aina yoyote. Matibabu haya hutolewa kwa malipo kwa waraibu wa dawa zote za kulevya kwa muda usiopungua miezi minne.
Serikali inaratibu uanzishwaji na kusimamia uendeshwaji wa Nyumba za Upataji Nafuu kwa kutumia Mwongozo wa Uanzishaji na Uendeshaji wa Nyumba za Upataji NafuuTanzania Bara. Hadi kufikia mwezi Februari 2022, kulikuwa na jumla ya nyumba 45 zinazotoa huduma hiyo katika mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Dares Salaam,Pwani, Dodoma, Morogoro, Iringa, Mwanza, Kagera, Tabora na Arusha.
Katika huduma hii watumiaji wa dawa za kulevya husaidiana wenyewe kwa wenyewe ambapo waraibu waliopata nafuu (kuacha matumizi ya dawa hizo kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja) huwaongoza waraibu wanaojiunga kushiriki mikutano ya Ustiri wa Mihadarati, (Narcotic
Anonymous) ambapo hupitishwa kwenye hatua kumi na mbili za upataji nafuu pamoja na unasihi. Waraibu wanaojiunga huweza hupatiwa mafunzo ya ujasiriamali, kazi za mikono pamoja na kushiriki katika shughuli za michezo.
ORODHA YA NYUMBA ZA UPATAJI NAFUU
Dar es salaam
Pillimisanah Foundation- (Back to life) People with Drug Dependence Relief Foundation (PEDEREF) (House of Wisdom) Drug Free Tanzania- (The ties that bind us recovery centre and Right Way) Stay Clean Foundation Kipepeo Foundation- (South Beach Sober house) New Vision of Life Society Morogoro Recovery Community Tanzania (MRC)- Kigamboni Changamoto ni Matumaini Pwani Life and Hope Rehabilitation Center The Light of Miracle Organization – (Women's Hope Rehabilitation) Dodoma TZ Sobriety and Rehabilitation Organization Morogoro Kipepeo Foundation – (Free at last sober house) Tanga Tanga Drug Free Courage and recovery Foundation GiftHope Foundation Kilimanjaro Kilimanjaro New Vision sober house and Sobriety Stay Clean Foundation- (Good Will Recovery Community) Arusha Tanzania Sobriety and Change Foundation Tanzania Sobriety Initiative Iringa Treatment centre for Drug & Alcohol Tabora Sober House Kagera Sobriety Forever Reh. Centre Zinatoa huduma gani? 1. Waraibu kukaa kwenye mazingira tulivu yasiyoruhusu matumizi ya vilevi vyovyote 2. Hupatiwa elimu na mafunzo ya kuacha kutumia dawa za kulevya na kupewambinu mbali mbali za kuishi bila kutumia dawa za kulevya kwa kufuata hatu 12 za upataji nafuu 3. Waraibu huishi humo kwa kipindi kisichopungua miezi minne. kuhufanya kazi mbali mbali za mikono na burudani. |
Jinsi ya kujiunga na nyumba hizo Mraibu unapoenda kwenye nyumba za upataji nafuu, hupewa maelekezo ya kujisajili na nyumba husika |
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya
S.L.P 80327
8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam
Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz
© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya