• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara

Madhara gani wanapata wanaotumia mbegu za bangi kama kiungo cha mboga?Madhara gani wanapata wanaotumia bangi kama mboga?

Bangi ni aina ya Dawa ya Kulevya inayotokana na Mmea uitwao Cannabis Sativoe. Majani ya Bangi yana Kemikali nyingi zinazoweza kuleta madhara katika mwili wa binadamu. Moja ya Kemikali ambayo imefanyiwa utafiti sana ni Tetrahydrocanabinoid(THC).

Matumizi ya Bangi husababisha utegemezi pamoja na madhara mengine ya kimwili na kiakili. Mbegu za Bangi hazina kiwango kikubwa cha THC hivyo matumizi ya Mbegu za Bangi kama kiungo cha mboga hayana madhara makubwa ya kiafya kulinganisha na uvutaji na majani.
Hata hivyo inashauriwa kuwa ikiwezekana watu watumie aina nyingine za viungo badala ya kutumia Mbegu za Bangi.

Dawa za kulevya zilizokamatwa hupelekwa wapi?

Dawa za kulevya zinazokamatwa hutunzwa kwenye Ghala maalum la kutunzia Vielelezo vya Kesi. Dawa hizi zinatakiwa kuwepo muda wote wa Kesi kama Kielelezo cha Kesi husika.

Pale Kesi zinapomalizika, Dawa hizi huteketezwa kwa taratibu zilizowekwa Kisheria. Tarehe 8 mwezi Oktoba .mwaka 2019 kiasi cha kilo 192 za Dawa za Kulevya aina ya Cocainei na Heroin zilichomwa katika Tanuru la kiwanda cha Cement Twiga kilichopo Wazo Hill baada ya Kesi zake kuisha.

je, Methadone ni dawa ya kulevya?

Methadone ni Dawa inayotumika kutibu watu walioathirika na Matumizi ya Dawa za Kulevya aina ya Heroin ili kuzuia Arosto wanayoweza kupata pindi wanapokosa Dawa ya Heroin.

Dawa hii hotolewa Hospitalini kwa maelezo ya Daktari. Iwapo mtu ataitumia kiholela inaweza kumletea madhara na hata kifo.

Methadone haiwezi kutumika kama Dawa ya Kulevya kwani haileti raha baada ya kuitumia kama ilivyo kwenye Dawa zingine za Kulevya.


Kwa nini Kuber na Ugoro haziko kwenye dawa za kulevya?

Kuberi na Ugoro ni bidhaa zinazotumiwa na watu wengi kwa ajili ya kujistarehesha. Bidhaa hizi ni aina ya vilevi visivyo dhibitiwa Kisheria. Kuber na ugoro zina viwango vya kemikali iitwayo Nicotine.

Mtu akitumia ugoro na kuberi huweza kumsababishia madhara kama;-
- Utegemezi,
- Saratani ya Mdomo, Fidhi na Koo na
- Mdomo kutoa harufu mbaya.

Kutokana na madhara hayo watu wanashauriwa kuachana na Matumizi ya Ugoro na Kuberi.

Majani ya Chamkwale hutumiwa mkoani Kigoma kama kilevi, Je yapo kwenye orodha ya dawa za kulevya?

Majani ya Chamkwale hutumiwa mkoani Kigoma kama kilevi, Je yapo kwenye orodha ya dawa za kulevya?

Je, kwenye kinywaji cha Cocacola kuna Cocaine?

Kinywaji cha Cocacola ni kinywaji kinachotumika dunia nzima. Kinywaji hiki kilianza kutengenezwa rasmi mwaka 1886. Kipindi hicho kinywaji hiki kilikuwa kinachanganywa na majani ya Coca yanayotummika kutengeneza Cocaine.

Kutokana na hali hiyo kulitokea malalamiko makubwa kutoka kwa jamii juu ya kuchanganya Cocaine kwenye Cocacola. Mwaka 1093 watengenezaji wa Cocacolawalipunguza kiasi kikubwa cha Cocaine kwenye kinywaji cha cocacola. Mwaka 1929 wanasayansi walifanikiwa kuondoa kabisa kiambata cha Cocaine katika cocacola.

Hivyo basi, kinywaji cha Cocacola kinachotumika sasa hivi hakina Cocaine.

Kwa nini Mirungi inaruhusiwa Kenya lakini hairuhusiwi Tanzania?

Kutokana na kemikali hizo katika mirungi, watumiaji wa mirungi wamekuwa wakipata madhara mbalimbali ya kimwili na kiakili. Baadhi ya madhara hayo ni;

 Huongeza kasi ya mapigo ya moyo hivyo kuweza kuongeza shinikizo la damu, kiharusi na hata kusababisha kifo.
 Husababisha vidonda vya utumbo mdogo, saratani ya mdomo, koo na tumbo
 Husababisha upungufu wa msukumo wa kufanya tendo la ndoa, kumaliza haraka na kutoweza kudumu kwenye tendo la ndoa kwa muda mrefu
 Hupunguza ubora wa mbegu za kiume na kuvuruga mfumo wa utokaji wake na hata kusababisha ugumba
 Mtumiaji hukosa usingizi na ulevi ukiisha mwilini husababisha usingizi mzito unaoweza kusababisha ajali hasa kwa madereva
 Huchochea ukatili, fujo, ugomvi, kuongea sana masuala ya kusadikika na kuhangaika.
 Mtumiaji hukosa kabisa hamu ya kula na kupungua uzito.
 Mirungi husababisha upungufu wa maji mwilini na kuleta tatizo la kukosa choo pamoja na ugonjwa wa bawasiri
 Mtumiaji mirungi akiikosa mirungi hupata uchovu, sonona, hasira za ghafla, kutetemeka, kushindwa kutulia na njozi za kutisha (night mares)
 Utumiaji mirungi huozesha meno na yale yanayosalia hubadilika rangi, fizi kuuma na harufu ya mdomo.
 Mirungi huharibu ufanisi wa ini mwilini katika kuchuja sumu za mwili
 Mirungi huamsha magonjwa ya akili yanayojitokeza kwa vipindi “mwezi mchanga” kwa watumiaji wenye tatizo hilo
 Matumizi ya mirungi wakati wa ujauzito yanaweza kusababisha kuzaliwa kwa watoto wenye uzito mdogo ambao huweza kukataa kunyonya kutokana na ladha ya maziwa kubadilishwa na viuatilifu vinavyotumika kwenye kilimo cha mirungi.


Kutokana na madhara hayo, kongamano la Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kupiga vita dawa za Kulevya na uhalifu (UNODC) la mwaka 1971 liliamua kuorodhesha Mirungi kuwa miongoni mwa dawa za kulevyana kupiga marufuku utafunaji wa mirungi. Kwa kuwa Tanzania ni Mwanachama wa umoja wa mataifa na tunaunga mkono kongamano hilo, tunawajibika kupiga marufuku matumizi ya mirungi.

Kitendo cha nchi nyingine kuhalalisha matuikzi ya mirungi siyo sababu ya kutufanya na sisi tuhalalishe. Kuna baadhi ya nchi zimehalalisha ndoa za jinsia moja, je na sisi tuige? Baadhi ya nchi za Ulaya ambazo awali ziiruhusu matumizi ya mirungi zimeanza kuiharamisha baada ya kuona madhara yake.



Dawa gani zinatumiwa sana?

Dawa gani zinatumiwa sana?

Nitamjiuaje mtumiaji

Nitamjiuaje mtumiaji

Habari Mpya

  • DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    Jan 25, 2023
  • Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za  kulevya zateketezwa

    Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za kulevya zateketezwa

    Dec 29, 2022
  • Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Dec 07, 2022
  • Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Oct 13, 2022
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya