• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

Mirungi

MIRUNGI NI NINI?

Mirungi ni aina ya dawa ya kulevya inayotokana na mmea unaoitwa “Catha edulis”. Mmea huo una kemikali za cathinone na cathine ambazo huongeza kasi ya utendaji wa mfumo wa fahamu. Mirungi ilikuwa inatumika tangu enzi za mababu kwenye nchi za pembe ya Afrika hususani Ethiopia, Eritrea, Kenya, Somalia pamoja na Rasi ya Arabuni nchini Yemen. Mirungi hutumika zaidi kwenye mikusanyiko ambayo hujumuisha zaidi wanaume ingawa katika miaka ya karibuni wanawake wamejiingiza katika matumizi. Nchini kwetu mirungi hustawi na hupatikana kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro- Same, Tanga- Lushoto na Arusha Mlima Meru. Kiasi kingi cha mirungi huingizwa nchini isivyo halali kutoka nchi jirani ya Kenya ambako ni zao halali la biashara. Mirungi hufahamika kwa majina ya gomba, veve, miraa, kangeta, mkokaa, colombo, asili, mbaga, alenle, nk.

MADHARA YA MIRUNGI

  • Huongeza kasi ya mapigo ya moyo hivyo kuweza kuongeza shinikizo la damu, kiharusi na hata kusababisha kifo.
  • Husababisha vidonda vya utumbo mdogo, saratani ya mdomo, koo na tumbo
  • Husababisha upungufu wa msukumo wa kufanya tendo la ndoa, kumaliza haraka na kutoweza kudumu kwenye tendo la ndoa kwa muda mrefu
  • Hupunguza ubora wa mbegu za kiume na kuvuruga mfumo wa utokaji wake na hata kusababisha ugumba
  • Mtumiaji hukosa usingizi na ulevi ukiisha mwilini husababisha usingizi mzito unaoweza kusababisha ajali hasa kwa madereva
  • Huchochea ukatili, fujo, ugomvi, kuongea sana masuala ya kusadikika na kuhangaika.
  • Mtumiaji hukosa kabisa hamu ya kula na kupungua uzito.
  • Mirungi husababisha upungufu wa maji mwilini na kuleta tatizo la kukosa choo pamoja na ugonjwa wa bawasiri
  • Mtumiaji mirungi akiikosa mirungi hupata uchovu, sonona, hasira za ghafla, kutetemeka, kushindwa kutulia na njozi za kutisha (night mares)
  • Utumiaji mirungi huozesha meno na yale yanayosalia hubadilika rangi, fizi kuuma na harufu ya mdomo.
  • Mirungi huharibu ufanisi wa ini mwilini katika kuchuja sumu za mwili
  • Mirungi huamsha magonjwa ya akili yanayojitokeza kwa vipindi “mwezi mchanga” kwa watumiaji wenye tatizo hilo
  • Wanawake wanaotumia mirungi kipindi cha ujauzito wana hatari ya kupata maumivu ya kifua, kuongezeka kwa mapigo ya moyo na msukumo wa damu
  • Matumizi ya mirungi yanaweza kusababisha kuzaliwa kwa watoto wenye uzito mdogo ambao huweza kukataa kunyonya kutokana na ladha ya maziwa kubadilishwa na viuatilifu vinavyotumika kwenye kilimo cha mirungi
  • Watumiaji mirungi hujikuta wakipenda kuvuta sigara au kunywa pombe wanapokosa usingizi hivyo kudhuru zaidi afya zao.
  • Mtumiaji wa mirungi hutumia fedha ambazo zingekidhi mahitaji ya familia kununulia mirungi hivyo kusababisha migogoro
  • Utafunaji mirungi hutumia muda mwingi na hufanyika muda wa kazi au muda ambao mtumiaji hutakiwa kujumuika na familia yake hivyo kushusha uzalishaji na ukaribu wa familia.

Sheria inasemaje kuhusu mirungi?

Mirungi katika taifa letu ni haramu.

Kujihusisha kwa namna yoyote na mirungi (kulima, kuuza, kuhifadhi, kutumia, nk)ni KOSA LA JINAI na adhabu yake inafikia hadi kifungo cha maisha

Baadhi ya nchi za Ulaya ambazo awali ziliruhusu matumizi ya mirungi zimeanza kuiharamisha baada ya kuona madhara yake

Utamsaidiaje mtumiaji wa mirungi

Mtumiaji anaweza kupunguza kiasi anachotumia taratibu na hatimaye kuacha.Aidha, asasi za kiraia huwasaidia watumiaji kuacha kwa kuwapa unasihi. Nyumba za upataji nafuu ‘sober house’ ambako hupitishwa kwenye hatua 12 za upataji nafuu. Kwa msaada zaidi tembelea tovuti www.dcea.go.tz

Ujumbe kwa jamii

  • Mirungi HAIONGEZI ufanisi kazini, ufaulu katika masomo, udereva wala nguvu za kiume
  • Wazazi na walezi wawalee watoto katika maadili mema ikiwemo kuwa nao karibu na kuwasikiliza
  • Vijana wajifunze na kuzingatia stadi za maisha
  • Epuka kutumia dawa za kulevya pamoja na kujiepusha na makundi hatarishi yanayoweza kukuingiza kwenye utumiaji

Habari Mpya

  • DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    Jan 25, 2023
  • Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za  kulevya zateketezwa

    Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za kulevya zateketezwa

    Dec 29, 2022
  • Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Dec 07, 2022
  • Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Oct 13, 2022
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya