(DCEA)
COCAINE NI NINI?
Ni dawa ya kulevya inayotokana na majani ya mmea unaojulikana kitaalam kama erythroxylum coca ambao hulimwa zaidi kwenye nchi ya Colombia ikifuatiwa na Peru na Bolivia. Asili ya dawa hii ni kuongeza kasi ya utendaji wa mfumo wa fahamu. Watumiaji hutumia cocaine kwa njia ya kunusa, kuvuta, kujidunga au kupaka ambapo huathirika na kuwa wateja wa dawa hiyo. Cocaine huwa katika hali ya unga mweupe au vijiwe vyeupe. Majina maarufu ya dawa hii yanayotumika mitaani ni pamoja na pele, diego, white sugar na sembe.
Unga wa cocaine na heroin huweza kufanana ingawa heroin hupatikana zaidi kuliko cocaine hapa nchini.
ATHARI ZA COCAINE
Kiafya:
Kijamii
Kiuchumi
Wanafunzi wengi wanaotumia cocaine hushindwa kuzingatia masomo yao na wengine kushindwa kumaliza shule. Vijana hawa hujikuta hawakubaliki katika jamii zao na kunyanyapaliwa hivyo hujiunga na magenge ya wahalifu.
Cocacola na cocaine
Kwenye miaka ya 1886 kinywaji cha Coca-Cola kilipoanzishwa kilikuwa na kiasi kidogo cha cocaine. Baada ya madhara ya cocaine kudhihirika katika jamii iliondolewa kwenye Coca-Cola mwaka 1903.
Sheria inasemaje kuhusu cocaine?
Kwa mujibu wa Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, sura ya 95, kujihusisha na cocaine kwa namna yoyote katika taifa letu ni KOSA LA JINAI. Kwahiyo, kusafirisha ndani na nje ya nchi, kuuza, kuhifadhi, kusambaza, kutumia na kutengeneza cocaine ni KOSA LA JINAI na adhabu yake inafikia hadi KIFUNGO CHA MAISHA JELA.
Utamsaidiaje mtumiaji wa cocaine
Mtumiaji anaweza kupunguza kiasi anachotumia taratibu na hatimaye kuacha.Aidha, asasi za kiraia huwasaidia watumiaji kuacha kwa kuwapa unasihi. Nyumba za upataji nafuu ‘sober house’ ambako hupitishwa kwenye hatua 12 za upataji nafuu. Kwa msaada zaidi tembelea tovuti www.dcea.go.tz
Ujumbe kwa jamii
1.Wazazi na walezi wawalee watoto katika maadili mema ikiwemo kuwa nao karibu na kuwasikiliza
2.Vijana wajitambue na kujiepusha na makundi hatarishi yanayoweza kuwaingiza kwenye utumiaji wa sigara, ugoro, pombe, shisha au bangi ambavyo watumiaji wengi wa cocaine wanakiri walianza navyo
3.Usijaribu kuonja cocaine kwani inaleta uraibu (uteja) kwa haraka na ni vigumu sana kuachana nayo.
4.Watumiaji wasinyanyapaliwe waelekezwe kwenye tiba
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya
S.L.P 80327
8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam
Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz
© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya