• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

Cocaine

J

COCAINE NI NINI?

Ni dawa ya kulevya inayotokana na majani ya mmea unaojulikana kitaalam kama erythroxylum coca ambao hulimwa zaidi kwenye nchi ya Colombia ikifuatiwa na Peru na Bolivia. Asili ya dawa hii ni kuongeza kasi ya utendaji wa mfumo wa fahamu. Watumiaji hutumia cocaine kwa njia ya kunusa, kuvuta, kujidunga au kupaka ambapo huathirika na kuwa wateja wa dawa hiyo. Cocaine huwa katika hali ya unga mweupe au vijiwe vyeupe. Majina maarufu ya dawa hii yanayotumika mitaani ni pamoja na pele, diego, white sugar na sembe.

Unga wa cocaine na heroin huweza kufanana ingawa heroin hupatikana zaidi kuliko cocaine hapa nchini.

ATHARI ZA COCAINE

Kiafya:

  • Hufanya mishipa ya damu kusinyaa na kuongeza msukumo la damu na mapigo ya moyo yasiyo na mpangilio hivyo kuleta shinikizo la damu, shambulizi la moyo, kiharusi au kifo cha ghafla
  • Huleta matatizo ya kiakili kama kujihisi unataka kudhuriwa, hasira, ukatili, vurugu, kukosa utulivu na kutaka kujiua.
  • Cocaine ikitumika kwa njia ya kunusa husababisha uwezo wa kunusa kupotea, pua kutoboka, mafua yasiyopona na kutoka damu puani.

J

  • Uvutaji wa cocaine ya mawe huharibu mapafu na kupata kikohozi kikali pamoja na kupumua kwa shida
  • Cocaine husababisha kusinyaa kwa mishipa ya damu kwenye mfumo wa chakula na utumbo kuoza
  • Cocaine huozesha meno kutokana na ongezeko la asidi na ukavu wa mdomo
  • §Hatari ya maambukizi ya homa ya ini, VVU na kifua kikuu kutokana na kushirikiana sindano, kubakwa, biashara ya ngono, kushiriki ngono zembe, kuishi mazingira yasiyo na hewa safi, nk.
  • Cocaine inapokosekana arosto hutokea na kupata uchovu mkali, usingizi, kutetemeka, kuhisi kutambaliwa na vitu mwilini, kutapika, kuwa dhaifu na kushindwa kuwa na utulivu. Arosto pia husababisha kukosa furaha, maumivu makali, kuharisha, homa, kukosa umakini na kuwa na hamu kubwa ya kutumia cocaine
  • Huweza kusababisha vifo kutokana na kuzidisha kiasi cha matumizi
  • Cocaine ikichanganywa na pombe huweza kusababisha kifo.
  • Kukosa usingizi na kuweza kusababisha ajali
  • Kukosa hamu ya kula na kusababisha afya kudhoofu
  • Utumiaji cocaine huchochea uvutaji wa sigara wa mfululizo

Kijamii

  • Mtumiaji kutowajibika na kushindwa kutimiza majukumu katika familia na kusababisha kuvunjika kwa ndoa, kutelekeza watoto na kwa watoto hufukuzwa na kuishi kwenye mageto
  • Ongezeko la vitendo vya uhalifu vikiwemo udokozi, unyang’anyi, utapeli pamoja na mmomonyoko wa maadili (biashara ya ngono).
  • Biashara ya dawa za kulevya huambatana na uhalifu mkubwa kwenye jamiikama ujangili, biashara ya binadamu, biashara haramu ya silaha, money laundering, utekaji, ugaidi, madanguro, nk

Kiuchumi

  • Matumizi ya dawa za kulevya hupunguza nguvu kazi ya taifa na kuongeza umasikini kwa familia na jamii kwa ujumla.
  • Biashara ya dawa za kulevya husababisha mzunguko wa fedha haramu, mfumuko wa bei, utakatishaji fedha, kukithiri kwa rushwa na kuongeza tofauti ya kipato
  • Serikali hutumia gharama kubwa kudhibiti tatizo la dawa za kulevya kwenye ukamataji, matibabu, kutoa elimu, nk

Wanafunzi wengi wanaotumia cocaine hushindwa kuzingatia masomo yao na wengine kushindwa kumaliza shule. Vijana hawa hujikuta hawakubaliki katika jamii zao na kunyanyapaliwa hivyo hujiunga na magenge ya wahalifu.

    Cocacola na cocaine

    Kwenye miaka ya 1886 kinywaji cha Coca-Cola kilipoanzishwa kilikuwa na kiasi kidogo cha cocaine. Baada ya madhara ya cocaine kudhihirika katika jamii iliondolewa kwenye Coca-Cola mwaka 1903.

    Sheria inasemaje kuhusu cocaine?

    Kwa mujibu wa Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, sura ya 95, kujihusisha na cocaine kwa namna yoyote katika taifa letu ni KOSA LA JINAI. Kwahiyo, kusafirisha ndani na nje ya nchi, kuuza, kuhifadhi, kusambaza, kutumia na kutengeneza cocaine ni KOSA LA JINAI na adhabu yake inafikia hadi KIFUNGO CHA MAISHA JELA.

    J

    Utamsaidiaje mtumiaji wa cocaine

    Mtumiaji anaweza kupunguza kiasi anachotumia taratibu na hatimaye kuacha.Aidha, asasi za kiraia huwasaidia watumiaji kuacha kwa kuwapa unasihi. Nyumba za upataji nafuu ‘sober house’ ambako hupitishwa kwenye hatua 12 za upataji nafuu. Kwa msaada zaidi tembelea tovuti www.dcea.go.tz

    Ujumbe kwa jamii

    1.Wazazi na walezi wawalee watoto katika maadili mema ikiwemo kuwa nao karibu na kuwasikiliza

    2.Vijana wajitambue na kujiepusha na makundi hatarishi yanayoweza kuwaingiza kwenye utumiaji wa sigara, ugoro, pombe, shisha au bangi ambavyo watumiaji wengi wa cocaine wanakiri walianza navyo

    3.Usijaribu kuonja cocaine kwani inaleta uraibu (uteja) kwa haraka na ni vigumu sana kuachana nayo.

    4.Watumiaji wasinyanyapaliwe waelekezwe kwenye tiba


Habari Mpya

  • DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    Jan 25, 2023
  • Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za  kulevya zateketezwa

    Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za kulevya zateketezwa

    Dec 29, 2022
  • Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Dec 07, 2022
  • Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Oct 13, 2022
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya