(DCEA)
HEROIN NI NINI?
Ni aina ya dawa ya kulevya inayotengenezwa na kemikali ya asili inayoitwa ‘morphine’ ambayo inapatikana kwenye utomvu ‘opium’ wa tunda la mmea wa afyuni ‘opium poppy’ unaolimwa zaidi kwenye nchi za Afghanstan, Myanmar na Laos. Hapa nchini, heroin inashika nafasi ya pili kwa matumizi baada ya bangi, na inatumiwa kwa njia ya kuvuta ikiwa imechanganywa na kiasi kidogo cha bangi na sigara au kwa njia ya kunusa na kujidunga. Heroin ni kati ya dawa za kulevya zinazoongoza kwa kusababisha uteja haraka, vifo vinavyotokana na kuzidisha kiasi cha matumizi au maradhi mbalimbali, pia ni dawa ambayo ina watumiaji wengi wanaohitaji tiba. Heroin hujulikana kwa majina ya mtaani kama unga, ngada, teli (cocktail), msharafu, white, kijiwe, brown, nk.
Utomvu ukivunwa kwenye mmea wa afyuni (opium)
MADHARA YA HEROIN
Kiafya
Kijamii
Kiuchumi
Kwa wanawake
Wanafunzi
Wengi wanaotumia heroin hushindwa kuzingatia masomo yao na wengine kushindwa kumaliza shule. Vijana hawa hujikuta hawakubaliki katika jamii zao na kunyanyapaliwa hivyo hujiunga na magenge ya wahalifu.
Sheria inasemaje ukijihusisha na heroin?
Kwa mujibu wa Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, sura ya 95, kujihusisha na heroin kwa namna yoyote katika taifa letu ni KOSA LA JINAI. Kwahiyo, kusafirisha ndani na nje ya nchi, kuuza, kuhifadhi, kusambaza, kutumia na kutengeneza heroin ni KOSA LA JINAI na adhabu yake inafikia hadi KIFUNGO CHA MAISHA JELA.
Utamsaidiaje mtumiaji wa heroin?
Mtumiaji anaweza kupunguza kiasi anachotumia taratibu na hatimaye kuacha.Wanaweza kupatiwa tiba ya methadone inayopatikana kwenye baadhi ya vituo vya afya. Aidha, asasi za kiraia huwasaidia watumiaji kuacha kwa kuwapa unasihi na huduma nyingine. Vilevile, nyumba za upataji nafuu ‘sober house’ huwasaidia kwa kuwapitisha kwenye hatua 12 za upataji nafuu.
Ujumbe kwa jamii
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya
S.L.P 80327
8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam
Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz
© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya