• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za kulevya zateketezwa

Imewekwa: Thursday 29, December 2022

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeshirikiana na wadau wengine muhimu kutoka Taasisi mbalimbali kuteteteza zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za kulevya zilizohusisha mashauri ya kuanzia mwaka 2009 hadi mwaka 2022. Veronica Matikila akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Kamisha Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gerald Kusaya amesema, uteketezaji huu uliofanyika uliofanyika katika kiwanda cha saruji cha Twiga Wazo jijini Dar es salaam, ni wa kawaida na hufanyika pale mashauri ya dawa za kulevya yanapomalizika mahakamani.

"Uteketezaji huu wa dawa za kulevya umefanyika kufuatia kumalizika kwa mashauri ya dawa za kulevya katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mahakama ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, na Mahakama za Hakimu Mkazi za Kisutu na Kibaha Pwani pamoja na Mahakama za Wilaya ya Kinondoni, Ilala, Temeke na Kigamboni" amesema Matikila.

Miongoni mwa dawa za kulevya zilizoteketezwa ni heroin kilo 569.25, kilo 15.3 za cocaine na tani mbili za bangi na mirungi.

Aidha, amesema hii ni mara ya pili kwa mwaka 2022 uteketezaji wa dawa za kulevya kufanyika. Uteketezaji wa kwanza ulifanyika mwezi Februari ambapo jumla ya kilo 250.7 ziliteketezwa katika kiwanda cha Saruji cha Dangote mkoani Mtwara. Kwa mwaka 2021, uteketezaji ulifanyika mkoani Mtwara ukihusisha kilo 355 za dawa za kulevya aina ya Methamphetamine. Pia, hekari 41 za mashamba ya bangi na mirungi ziliteketezwa katika mikoa ya Pwani, Arusha na Kilimanjaro.

Matikila ameongeza kuwa, hii ni mara ya tatu kufanya uteketezaji katika kiwanda hiki cha Twiga tangu kuanzishwa kwa Mamlaka mwaka 2017. Mara ya kwanza uteketezaji ulifanyika tarehe 8 Oktoba, 2019 ambapo kilo 120.91 za heroin, kilo 70.96 za cocaine ziliteketezwa. Mara ya pili ulifanyika tarehe 12 Novemba, 2020 ambapo kilo 118.174 za heroin, kilo 3.932 za cocaine na kilo 120 za bangi ziliteketezwa.

Amefafanua kwamba, uteketezaji wa dawa za kulevya hufanyika kwa namna ambayo hulinda afya na kuzingatia kanuni za utunzaji wa mazingira huku ukishuhudiwa na wadau muhimu. “Wadau hao ni Hakimu au Jaji, Kamishna Jenerali, Inspekta Jenerali wa Polisi, Mkurugenzi wa Mashtaka, Mkemia Mkuu wa Serikali, Idara ya Usalama wa Taifa, Baraza la Taifa la Mazingira na wadau wengine watakaoalikwa na Kamishna Jenerali” amefafanua Matikila.

Kipekee amewashukuru Majaji na Mahakimu, Inspekta Jenerali wa Polisi, Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini, Mkemia Mkuu wa Serikali, Idara ya Usalama wa Taifa, Baraza la Taifa la Mazingira, Waandishi wa Habari na wadau wengine walioshiriki katika kufanikisha zoezi hili muhimu la uteketezaji pamoja na mwekezaji wa Kiwanda cha Saruji cha Twiga kwa kuendelea kutoa ushirikiano na kuruhusu zoezi hili kufanyika kiwandani kwake.

Habari Mpya

  • DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    Jan 25, 2023
  • Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za  kulevya zateketezwa

    Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za kulevya zateketezwa

    Dec 29, 2022
  • Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Dec 07, 2022
  • Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Oct 13, 2022
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya