• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

Imewekwa: Wednesday 07, December 2022

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata kilo 16.643 za dawa ya kulevya jijini Dar es Salaam.

Kati ya dawa hizo,kilo 15.19 ni heroin, gramu 655.73 za cocaine na gramu 968.67 ni dawa za kulevya aina ya Methamphetamine zilizowahusisha jumla ya watuhumiwa saba.

Hayo yamebainishwa leo Disemba 7, 2022 na kamishna jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gerald Musabila Kusaya wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Kamishna Kusaya amesema kuwa, Ukamataji wa kilo 15.19 za dawa za kulevya aina ya heroin zilizowahusisha watuhumiwa watatu ni mwendelezo wa operesheni zilizopita. “Watuhumiwa hawa ni washirika wa Kambi Zuberi Seif na wenzake waliokamatwa wakiwa na kilo 34.89 za heroin katika operesheni ya mwanzoni mwa mwezi Novemba 2022,” amesema Jenerali Kusaya.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Suleman Thabit Ngulangwa mwenye umri wa miaka 36 ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa Salasala, Sharifa Seleman Bakar mwenye umri wa miaka 41 ambaye ni mkazi wa Maji matitu - Mbagala na Farid Khamis Said umri miaka 22 na mkazi wa Maji matatu, Mbagala na wote ni wakazi wa Dar es Salaam.


u

Wakati huo huo, Kamishna Jenerali Kusaya amewataja watuhumiwa wengine wanne waliokamatwa na gramu 655.75 za cocaine na gramu 968.67 za Methamphetamine wakiwa kwenye harakati za kusafirisha dawa hizo za kulevya kwenda nje ya nchi.

Watuhumiwa hao wanne ni Hussein Rajab Mtitu mwenye umri wa miaka 28 anayejulikana pia kama Chodri Mohamed ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa Kibonde maji, Mbagala. Mwingine ni Jaalina Rajab Chuma mwenye umri wa miaka 31 anayejulikana pia kama Jaalina Mohan ambaye ni mjasiriamali na mkazi wa Tandika, mwingine ni Shabani Abdallah Said mwenye umri wa miaka 36 na mkazi wa Kilimahewa, Tandika, hawa pia ni wakazi wa Dar es Salaam.

“Mtuhumiwa mwingine ni Irene Dickson Mseluka mwenye umri wa miaka 39ambaye yeye ni mfanyabiashara na mkazi wa Ndala Shinyanga. Watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa na watafikishwa mahakamani mara baada ya taratibu za kiupelelezi kukamilika” amesema Jenerali Kusaya.

Pamoja na hayo, kamishna jenerali Kusaya ametunia nafasi hiyo kuwaonya wasanii wanaotumia na wanaohamasisha matumizi ya dawa za kulevya kupitia kazi zao za sanaa akiahidi kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

“kuna wasanii wanahamasisha matumizi ya dawa za kulevya. Wengine wanahamasisha matumizi ya bangi lakini hili tutalifanyia kazi. Kama kuna wasanii wanaotunga nyimbo ambazio sio za kuelimisha jamii badala yake wanatunga nyimbo za kuhamasisha matumizi ya dawa za kulevya tutawachukulia hatua kwa mujibu wa sheria” amesema Jenerali Kusaya.

Aidha, amewaomba waandishi kutumia taaluma yao kuwaeleza watanzania madhara ya dawa za kulevya.


Mwisho

Habari Mpya

  • DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    Jan 25, 2023
  • Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za  kulevya zateketezwa

    Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za kulevya zateketezwa

    Dec 29, 2022
  • Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Dec 07, 2022
  • Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Oct 13, 2022
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya