• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

DCEA na TAKUKURU Kushirikiana

Imewekwa: Wednesday 19, April 2023

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), wamekubaliana kushirikiana katika kuimarisha mapambano dhidi ya tatizo la dawa za kulevya na kupiga vita vitendo vya rushwa Nchini.

Taasisi hizo zimefikia maamuzi hayo baada ya kubaini kuwa wafanyabiashara wa dawa za kulevya kwa kiasi kikubwa hutumia rushwa kufanikisha usafirishaji wa dawa za kulevya kwa kuwashawishi watu wasio waaminifu ili wawasaidie kukamilisha uharifu huo katika maeneo mbalimbali nje na ndani ya nchi.

Ushirikiano baina ya DCEA na TAKUKURU utajikita zaidi katika utoaji wa elimu juu ya tatizo la dawa za kulevya na kupiga vita rushwa kwa wanafunzi kuanzia shule za msingi hadi vyuoni kupitia vilabu vya kupiga vita rushwa mbazo sasa zitatumika kupiga vita rushwa na dawa za kulevya.

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Aretas Lyimo amesema, Mamlaka ya Kuidhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imeona ni vema ikashirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili kupanua wigo wa elimu juu ya tatizo la dawa za kulevya.

"Ushirikiano huo ni muhimu kwani utaisaidia sehemu kubwa ya jamii hasa wanafunzi ambao baadhi yao kujiingiza kwenye matumizi ya dawa za kulevya wakiwa katika umri mdogo, kufahamu madhara ya dawa za kulevya na hatimaye kutoshiriki kwenye matumizi na biasha ya dawa hizo' amesema kamishna jenerali Lyimo..

Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa CP. Salum Rashid Hamduni, amebainisha kuwa, anatambua ushirikiano baina ya Taasisi hizi utaleta tija katika mapambano dhidi ya Rushwa na tatozo la dawa za kulevya nchini hivyo ni muhimu taasisi hizo zikajipanga kikamilifu katika kuhakikisha kuwa jukumu hilo linatekelezwa kwa ufanisi mkubwa.

Aidha, amesema kuwa, ushirikino huo usijikite tu katika utoaji wa elimu juu ya Rushwa na Dawa za kulevya bali pia katika kubadilishana uzoefu wa namna ya kukabiliana makosa ya rushwa, kwani ni wazi kuwa, idadi kubwa ya watu wanaokutwa na makosa hayo pia hukutwa na makosa ya rushwa na uhujumu uchumi.

Makubaliano hayo yamefanyika jijini Dodoma, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAKUKURU yaliyohudhuriwa pia na baadhi ya Maafisa kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.


f

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa CP. Salum Rashid Hamduni (kulia) akisisitiza jambo wakati wa kikao na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya - DCEA (kushoto).


f

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa CP. Salum Rashid Hamduni (kulia) akimkabidhi zawadi Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za KUlevya Aretas Lyimo (kushoto) walipotembelea ofisi za TAKUKURU Dodoma.



f

Kamishna wa Kinga na Tiba kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dkt. Perter Patrick Mfisi (aliye nyoosha mkono) akiwasilisha jambo katika kikao hicho.

Habari Mpya

  • Waendesha mashtaka wa Serikali  na wapelelezi wanolewa juu ya upelelezi na  uendeshaji wa mashauri ya dawa za kulevya

    Waendesha mashtaka wa Serikali na wapelelezi wanolewa juu ya upelelezi na uendeshaji wa mashauri ya dawa za kulevya

    Jul 31, 2023
  • DCEA yafanya ziara uwanja wa ndege wa Julius Nyerere

    DCEA yafanya ziara uwanja wa ndege wa Julius Nyerere

    Jul 23, 2023
  • Hekari101 na Magunia 482 ya bangi yateketezwa Arusha

    Hekari101 na Magunia 482 ya bangi yateketezwa Arusha

    Jun 01, 2023
  • DCEA, TAKUKURU kuunganisha nguvu kupinga rushwa na dawa za kulevya

    DCEA, TAKUKURU kuunganisha nguvu kupinga rushwa na dawa za kulevya

    May 26, 2023
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya