Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Waziri Mkuu

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

( DCEA )

Tani 9.93 za Dawa za Kulevya na Chupa 1,795 za Dawa Tiba Zenye Asili ya Kulevya Zakamatwa Nchini

04 March, 2026 Pakua

Mwezi Januari na Februari 2026, Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imekamata tani 9.93 za dawa za kulevya aina mbalimbali, chupa 1,795 za dawa tiba zenye asili ya kulevya na kuteketeza ekari 87.5 za mashamba ya bangi. Magari 6 na pikipiki 29 vilikamatwa katika operesheni hizo huku watuhumiwa 151 wakikamatwa kuhusika na uhalifu huo.