Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Waziri Mkuu

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

( DCEA )

Kilogramu 767.2 za Dawa za Kulevya Zakamatwa Nchini

22 April, 2024 Pakua

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), imekamata jumla ya Kilogramu 767.2 za dawa za kulevya katika operesheni zilizofanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, na Tanga kuanzia tarehe 4 hadi 18 Aprili 2024. Kati ya dawa zilizokamatwa, heroin ni kilogramu 233.2, methamphetamine kilogramu 525.67 na skanka kilogramu 8.33. Watuhumiwa 21 wamekamatwa kuhusika na dawa hizo za kulevya, baadhi yao wamefikishwa mahakamani na wengine watafikishwa taratibu za kisheria zitakapokamilika.