• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

Operesheni Teketeza Mashamba ya bangi Arusha; Kamishna Jenerali Kusaya Azungumza

Imewekwa: Thursday 26, May 2022

Mamlaka ya Kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) kwa kushirikiana na Vyombo vya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Arusha, imeteketeza zaidi ya hekari 21 za mashamba ya bangi mkoani humo. Sambamba na uteketezaji huo, takribani kilo 720 za bangi zilikamatwa katika matukio mbalimbali, yaliyowahusisha wafanyabiashara wanne ambao wanashikiliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari tarehe 24 Mei, 2022 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gerald Musabila Kusaya alieleza kuwa tarehe 20 Mei 2022 Mamlaka ilianza operesheni maalum katika wilaya ya Arumeru na Monduli mkoani Arusha iliyolenga kupambana na dawa za kulevya aina ya bangi na kuwasaka watu wote wanaomiliki mashamba ya bangi pamoja na wale wanaojihusisha kwa namna yoyote na biashara ya dawa za kulevya aina ya bangi.

‘’Tumefanikiwa kuwakamata wafanyabiashara ambao walikuwa wakisafirisha magunia ya bangi ambayo ni zaidi ya kilo 720. Katika operesheni hiyo jumla ya watuhumiwa wanne tumewakamata. Hawa ni wanaomiliki mashamba na tuliowakuta na magunia ya bangi wakiyasafirisha kutoka Monduli na Arumeru kuja jijini Arusha” amesema Kamishna Jenerali Kusaya.

Aidha, amesema operesheni hizi zitakuwa endelevu katika maeneo yote Nchini kuhakikisha aina zote za dawa za kulevya zinadhibitiwa. Ameendelea kusema kuwa, kwa hali ilivyo katika maeneo mbalimbali Nchini hususani mkoa wa Arusha bado anaimani yapo mashamba ya bangi pamoja na baadhi ya wananchi waliohifadhi magunia ya dawa hizo.

Vilevile, ametoa onyo kali kwa wananchi wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya, kuachana na biashara hiyo na kutafuta biashara halali itakayompatia kipato, kwani Mamlaka haitawafumbia macho.

Pia, amewaomba wananchi kuendelea kushirikiana na Mamlaka pamoja na Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa kutoa taarifa ‘’Jukumu lenu ninyi wananchi tuambieni nani,yupo wapi. anafanya nini na anajihusishaje na dawa za kulevya, sisi kama vyombo vya ulinzi na usalama tutakachokifanya taarifa yeyote ile tutakayoipokea tutaifanyia kazi kikamilifu ili wale wote wanaojihusisha na dawa za kulevya tuweze kuwatia mbaroni, wafikishwe kwenye vyombo vya sheria na hatimaye kuhukumiwa kulingana na makosa yao” amesema Kusaya.

Pamoja na hayo, Kamishna Kusaya amewataka wasanii mbalimbali Nchini kutumia Sanaa zao kutoa ujumbe wenye elimu katika jamii na siyo kuhamasisha uvutaji wa bangi, kwani katika uimbaji wao au uandaaji wa muziki huwa kuna maigizo mbalimbali wanayafanya hivyo yaelekezwe katika kuelimisha jamii na siyo vinginevyo. ‘’Wasanii wetu wamekuwa wakifanya maigizo mbalimbali katika nyimbo zao, tunawaomba watumie vyema nafasi hiyo kwaajili ya elimu ya kuifunza jamii na isiwe vinginevyo, ikiwa kinyume tutawachukulia hatua za kisheria, Tunataka tuwe na Tanzania huru isiyokuwa na dawa za kulevya''. alisema Kusaya

Dawa za kulevya zinaweza kwisha pale ambapo kila Mtanzania atazichukia dawa hizo,huku akisema dawa hizo zina madhara kwa Taifa zima endapo kama biashara hiyo itakuwa inaendelea bila kutazama kwamba kuna athari gani nyuma yake’ amesisitiza Kamishna jenerali Kusaya.

s

Baadhi ya magunia ya dawa za kulevya aina ya bangi yaliyokamatwa


s

Kamishna Jenerali Gerald Kusaya alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari mkoani Arusha


s

Moja ya shamba lililoteketezwa katika operesheni tokomeza bangi mkoani Arusha

Habari Mpya

  • DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    Jan 25, 2023
  • Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za  kulevya zateketezwa

    Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za kulevya zateketezwa

    Dec 29, 2022
  • Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Dec 07, 2022
  • Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Oct 13, 2022
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya