• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

Kamishna jenerali Lyimo kuanza na vijiwe vyote, vita dhidi ya dawa za kulevya

Imewekwa: Wednesday 19, April 2023

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas James Lyimo ametaja malengo yake katika kupambnana na dawa za kulevya nchini. Kamishna Lyimo ameyasema hayo mbele ya waandishi wa habari tarehe 1 aprili, 2023 mkoani Mtwara kwenye tukio la uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ambapo Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imeshiriki kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara yamatumizi na biashara ya dawa za kulevya.

“Mimi kama kamishna mpya wa Mamlaka hii, malengo yangu niliyoingia nayo ni kuhakikisha tunadhibiti kabisa uingizaji na usambazaji wa dawa za kulevya nchini. Kwahiyo nitoe wito kwa watumiaji wa dawa za kulevya kuacha kutumia dawa hizo lakini pia wale wauzaji na wasambazaji wa dawa hizi kuacha kabisa biashra hiyo kwani tunafanya operesheni kabambe nchi nzima, na tutahakikisha vijiwe vyote vya wauzaji , na watumiaji wa dawa za kulevya vinasambaratishwa” Amesema kamishna jenerali Lyimo.

“Tutafafanya operesheni nchi nzima na tutawakamata wanaofanya biashara ya dawa kulevya. Lakini pia tutafanya operesheni kijiji kwa kijiji mikoa yote kuhakikisha kwamba wale wote wanaolima bangi na mirungi tunawakamata na kuteketeza mashamba yao. Kwa hiyo nitoe wito kwa wananchi, mashirika ya dini na serikali kwa ujumla kuhakikisha kwamba tunatoa taarifa wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ili kuweza kufanikisha operesheni mbalimbalikatika kudhibiti dawa za kulevya”amefafanu Kamishna Jenerali Lyimo.

Aidha, ametoa wito kwa jamii kutambua kuwa ushirikiano wao utaiwezesha nchi kuwa salama na huru bila dawa za kulevya, kwani dawa za kulevya zina madhara makubwa sana kijamii, kiafaya, kimazingira na kiuchumi kwani zinapotezaq huchangia kupoteza nguvu kazi ya Taifa.

Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa zimezinduliwa na waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tainzania Mhe. Kassim MajaliwaMajaliwa mkoani Mtwara katika uwanja wa Nangwanda sijaona, ambapo Mamlaka ya Kudhibi na Kupambana na Dawa za Kulevya imeshiriki katika utoaji wa elimu kwani ina ujumbe wa kudumu katika mbio hizo.

s

Maofisa wa Mamlaka wakitoa elimu ya dawa za kulevya kwenye maonesho ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge katika viwanja vya Sabasaba mkoani Mtwara


“Sisi ni sehemu ya Mwenge, na kwa sababu mwenge unatembea nchi nzima kwa ajili ya kukemea maovu na kuhakikisha kuwa maovu yanaondoka kwenye jamii; dawa za kulevya ni moja ya maovu yanayokemewa na mwenge hivyo tuko hapa kuitaka jamii iachane na matumizi ya dawa za kulevya na mwisho wa siku kuhakikisha tunakuwa na Tanzania isiyojihusisha na biashara wala matumizi ya dawa za kulevya” amesema Kamishana Jenerali Aretasi Lyimo aliyeteuliwa mwishoni mwa Mwezi Machi, 2023 na Rais wa Jamhauri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani Kuiongoza Mamlaka na Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya.


j

Kamishna Jenerali Aretas Lyimo akizungumza na waandishi wa habari

Habari Mpya

  • Waendesha mashtaka wa Serikali  na wapelelezi wanolewa juu ya upelelezi na  uendeshaji wa mashauri ya dawa za kulevya

    Waendesha mashtaka wa Serikali na wapelelezi wanolewa juu ya upelelezi na uendeshaji wa mashauri ya dawa za kulevya

    Jul 31, 2023
  • DCEA yafanya ziara uwanja wa ndege wa Julius Nyerere

    DCEA yafanya ziara uwanja wa ndege wa Julius Nyerere

    Jul 23, 2023
  • Hekari101 na Magunia 482 ya bangi yateketezwa Arusha

    Hekari101 na Magunia 482 ya bangi yateketezwa Arusha

    Jun 01, 2023
  • DCEA, TAKUKURU kuunganisha nguvu kupinga rushwa na dawa za kulevya

    DCEA, TAKUKURU kuunganisha nguvu kupinga rushwa na dawa za kulevya

    May 26, 2023
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya