• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

Imewekwa: Wednesday 25, January 2023

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gerald Musabila Kusaya amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Disemba 2021 mpaka sasa jumla ya watumiaji 12,800 wa dawa za kulevya wameamua kuachana na matumizi hayo na kukubali kwenda katika vituo vya Methadone kwa ajili ya kutibiwa.

Kamishina Jenerali Kusaya amesema hayo katika maonyesho ya wiki ya sheria yanayofanyika jijini Dodoma Katika viwanja vya Nyerere (Nyerere Square) alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa idadi ya waathirika waliojitokeza kupata tiba ni matokeo ya kazi kubwa inayofanywa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya hasa katika kutoa elimu kwa wananchi juu ya tatizo la dawa za kulevya ikiwa ni pamoja na Kudhibiti matumizi na Kupambana na biashara ya dawa hizo.

“Mamlaka imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi kuhusiana na Sheria za dawa za kulevya pamoja na madhara yatokanayo na dawa hizo. Matumizi na biashara ya dawa za kulevya yamepungua kwa kiasi kikubwa, wengi wameacha na wengine wameamua kujisalimisha ili kupata matibabu katika vituo vya serikali” amesema Kamishna Jenerali Kusaya.

Akiendelea kubainisha hayo, amesema Tanzania imefanya vizuri zaidi kwa nchi za Afrika Mashariki katika eneo la kutoa matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya ambapo mpaka sasa kuna vituo vya Methadone 15 nchi nzima.

Aidha, amebainisha kuwa kutokana na uimara katika udhibiti wa dawa za kulevya, watumiaji wa dawa za hizo wamebuni mbinu mpya na kuanza kutumia dawa tiba zenye asili ya kulevya kama mbadala wa dawa za kulevya.

“Matumizi ya heroin, bangi na mirungi yamepungua kwa kiasi kikubwa, sasa hivi wameanza kutumia dawa tiba za binadamu kama vile Valium, Tramadol, Ketamine na nyinginezo, kama mbadala lakini wapo pia wanaotumia rangi, na petroli na gundi" amesema Jenerali Kusaya.

Pia, amesema Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya itaendelea kudhibiti uingizwaji kemikali bashirifu ambazo zikichepushwa zinaweza kutumika kutengeneza dawa za kulevya pamoja na kuimarisha ushirikiano na vyombo vingine vikiwemo Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TMDA) ili kuona namna ya kufanya kuhusu matumizi ya shisha, rangi na petrol.

Pamoja na hayo, Kamishna jenerali Kusaya amesema kuwa kwa kipindi cha Disemba 2021, mpaka Disemba 2022 Mamlaka imefanikiwa kuzuia uingizwaji wa kilo 120 na lita 85 za kemikali bashirifu.

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya ni moja ya wadau wanaoshiriki katika Maonesho ya Wki ya Sheria jijini Dodoma, iliyofunguliwa tarehe 22 mwezi Januari, 2023 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Isdor Mpango na yanatarajiwa kufikia tamati tarehe 29 ya mwezi huu.

Habari Mpya

  • DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    DCEA yashiriki Maonesho Wiki ya Sheria

    Jan 25, 2023
  • Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za  kulevya zateketezwa

    Zaidi ya tani mbili na nusu za dawa za kulevya zateketezwa

    Dec 29, 2022
  • Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Kilo 16.643 za Dawa za Kulevya Zakamatwa jijini Dar es Salaam

    Dec 07, 2022
  • Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Serikali Yaomba Viongozi wa Dini Kukemea Matumizi ya Dawa za Kulevya

    Oct 13, 2022
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya