• Wadau Wetu
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Barua Pepe Ya watumishi
  • English
    English

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

(DCEA)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Tunafanya nini?
    • Misingi Mikuu
    • Sisi ni nani
    • Muundo wa Taasisi
  • Dawa za kulevya
    • Ukweli kuhusu Cocaine
    • Ukweli kuhusu Heroin
    • Ukweli kuhusu Mirungi
    • Ukweli kuhusu Bangi
  • Ukaguzi na Sayansi Jinai
    • Kemikali Bashirifu
      • Jedwali la kemikali bashirifu
      • Udhibiti wa kemikali bashirifu
    • Dawa mpya za kulevya
      • Dawa mpya za kulevya ni nini?
      • Orodha ya dawa mpya za kulevya
    • Nakotiki na Saikotropiki
      • Nakotiki na Saikotropiki ni nini?
      • Dawa zinazodhibitiwa
    • Miradi
      • Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika udhibiti wa kemikali bashirifu
      • Maabara ya sayansi jinai
  • Vituo Tiba
    • Huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
    • Vituo tiba kwaajili ya waathirika wa dawa za kulevya
    • Nyumba za upataji nafuu
  • Machapisho
    • Sheria na Kanuni
    • Miongozo
    • Vipeperushi
    • Mada mbalimbali
    • Taarifa za Mwaka za Dawa za Kulevya
    • Taarifa za Hesabu za Mwaka
    • Tuzo
    • Hotuba
    • Elimu kwa Umma
    • Magazeti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha za Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Magazeti

DCEA yafanya ziara uwanja wa ndege wa Julius Nyerere

Imewekwa: Sunday 23, July 2023

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo akiambatana na viongozi wengine wa Mamlaka, amefanya ziara ya kikazi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kufanya kikao na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya uwanja huo kwa lengo la kujadili na kubadilishana uzoefu wa kiutendaji utakaosaidia kudhibiti usafirishaji na uingizaji wa dawa za kulevya nchini kupitia uwanja huo.

Akizungumza wakati wa kikao hicho kamishna Lyimo amesema lengo kuu la ziara hiyo ni kujitambulisha kwani anatambua JNIA ni wadau muhimu wa Mamlaka na wanashirikiana katika kazi. Pia, ziara hiyo ni muhimu katika kuimarisha ushirikano kati ya Mamlaka na viwanja wa ndege ili kupambana na dawa za kulevya kwani baadhi ya waharifu wa dawa za kulevya wanatumia viwanja vya ndege kuingiza na kutoa dawa hizo.

“Viwanja vya ndege ni vituo muhimu sana katika udhibiti wa dawa za kulevya kwa kuwa duniani kote viwanja vya ndege hupitisha dawa za kulevya. kwahiyo tukiimarisha mahusiano na kushirikiana tunaweza kulimaliza hili tatizo. Amesema Kamishna Jenerali Lyimo.

Aidha, amewaomba watumishi wa uwanja wa ndege kushiriki katika mapambano kwa kutoa taarifa za watu wanaosafirisha dawa hizo ikiwa ni pamoja na kutoa ushahidi mahakamani pale inapohitajika.

“Kuna kesi ambazo tunazianzisha zikitokea airport, sasa kuna wale maafisa wa airport ambao huwa wanashuhudia tunaomba wasiwe na wasiwasi kwenda mahakamani kutoa ushahidi, pia wawe wanatoa taarifa kwetu pale wanapowabaini waharifu wa dawa za kulevya. Mtoa taarifa awe na uhakika kwamba taarifa yake italindwa na hakuna mtu atakayemjua kwamba ni yeye aliyetoa taarifa” amesema kamishna Jenerali Lyimo.

Nae Kamishna wa Kinga na Tiba Dkt. Peter Mfisi amesema ni muhimu kujua nchi inatumia rasilimali nyingi kupambana na dawa za kulevya kutokana na madhara yanayotokana na matumizi na biashara ya dawa hizo.

Hivyo, ameomba kupata nafasi ya kutoa elimu mara kwa mara kwa watumishi wa uwanja wa ndege kuwaeleza jinsi ya kugundua dawa za kulevya, Pamoja na madhara dawa hizo katika nyanja zote za maisha ili waweze kuelewa umuhimu wa kupambana na dawa za kulevya na kuchukua hatua pale wanapowabaini wanaosafirisha dawa za kulevya.

“Nchi yetu ni kama transit country, dawa zinaingia na kutoka, lakini zinapotoka kuna nyingine nyingi zinabaki kwahiyo unapomuona mtu anasafirisha dawa za kulevya Kwenda nje ujue na hapa nchini anauza. Hivyo, ukimkamata utamfanya asizisafirishe kule anakozipeleka na asiziuze huku kwa watu wetu” amesema Dkt. Mfisi.

Kwa upande wa mkurugenzi wa JNIA Bi. Rehema Myeya amesema wako tayari na wanahitaji sana kupata mafunzo kutoka DCEA kwa ajili ya kuwasaidia maafisa wao kupata uelewa kuhusu dawa za kulevya. Pia amesisitiza umuhimu wa kubadirishana taarifa kati ya DCEA na JNIA ili kufanikisha azma njema ya kupambana na uhalifu.

Ameongeza kuwa unyeti wa suala la dawa za kulevya linahitaji watu wote kuwa wazaendo kwani nchi yoyote inafanikiwa kutokana na uzalendo.

“Wakati mwingine mtu anapanda ndege akiwa free anaenda kumeza dawa kiwanja kingine, na inatokea anakamatwa huko nje na anakuwa anachafua taswira ya nchi” Amesema Rehema.

Pamoja na majadiliano mengone, Mamlaka na Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya na Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere wamekubaliana kushughulikia chngamoto zilizobainika zinazokwamisha juhudi za mapambano.

MWISHO.

Habari Mpya

  • DCEA yatua Tarime kwa kishindo: Yawachachafya wakulima wa bangi bonde la mto Mara

    DCEA yatua Tarime kwa kishindo: Yawachachafya wakulima wa bangi bonde la mto Mara

    Nov 01, 2023
  • Gunia 131 za bangi zakamatwa Morogoro

    Gunia 131 za bangi zakamatwa Morogoro

    Nov 01, 2023
  • Waendesha mashtaka wa Serikali  na wapelelezi wanolewa juu ya upelelezi na  uendeshaji wa mashauri ya dawa za kulevya

    Waendesha mashtaka wa Serikali na wapelelezi wanolewa juu ya upelelezi na uendeshaji wa mashauri ya dawa za kulevya

    Jul 31, 2023
  • DCEA yafanya ziara uwanja wa ndege wa Julius Nyerere

    DCEA yafanya ziara uwanja wa ndege wa Julius Nyerere

    Jul 23, 2023
  • Soma Zaidi

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya
Tanzania Census 2022

Mawasiliano

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

S.L.P 80327

8 Barabara ya Kivukoni Front, 11486 Dar es salaam
Dar es Salaam

Simu: +255 22 211 3754/57
Nukushi: +255 22 211 3752
Barua pepe: cg@dcea.go.tz

Nifanyaje?

  • Nitatoaje taarifa ya uhalifu wa dawa za kulevya na matumizi?
  • Nitapataje huduma ya matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya
  • Nitapataje huduma ya Nyumba ya Upataji Nafuu kwa waathirika wa dawa za kulevya

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Utumishi
  • Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)
  • Hospitali ya Taifa Muhimbili
  • Wakala ya Serikali Mtandao

Kurasa za Karibu

  • picha za Mamlaka
  • Kauli mbiu ya siku
  • Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
  • Mafunzo
  • Ukamataji
  • Taarifa ya board

© 2023 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Haki zote zimehifadhiwa..
Imesanifiwa, Imetengenezwa, na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Inaendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya